Ngarisha Ngozi yako kwa Nguvu ya Asili na Kuifanya iwe Laini na Ng'avu Boresha afya ya Ngozi kwa Tiba isiyo na Mazara
Wekeza katika ngozi yako kwa kuwa itakuwa ikikuwakirisha mbele za watu kwa muda mrefu
Program Hii itaondoa Mikunjo na Kukuweka Mrembo siku Zote
Tunaboreshaje Afya ya ngozi yako
Vitu vingi tunavyoviona juu ya ngozi zetu ni matokeo ya vile vinavyoendelea ndani uzuri wa ngozi yako na ubora wake vinahusiana sana na afya ya mwili wako kwa ujumla
Program yetu inaondoa chunusi
Huondoa madoa ya chunusi
Huondoa makunyanzi yote katika mwili mzima
Hulainisha ngozi nakuifanya nyororo
Hupunguza kasi ya uzee
Hukupa unyevu wakudumu kwenye ngozi
Huondoa fangasi za ngozi mapajani na vidoleni
Huipa kinga ngozi yako kuathirika na miale ya jua
Huipa ngozi elasticity na kuifanya iwe nyororo na wakati huo huo bado ni imara
---------------------------------------------
Jinsi ambavyo chunusi Utokea
Chunusi ni katika matatizo ya ngozi ambayo huathiri watu wengi wakati fulani. Husababisha madoa, ngozi ya mafuta na wakati mwingine ngozi ambayo ukiigusa unahisi hisia za moto au uchungu. Chunusi (kwa Kiingereza: acne vulgaris) ni hali ya muda mrefu ya ngozi inayodhihirika kwa madoa meusi, madoa meupe, ngozi yenye mafuta na wakati mwingine kovu.
Chunusi ni ugonjwa wa ngozi ambao hujitokeza kama viuvimbe/vipele vidogo vidogo hasa sehemu za uso, kifuani na hata mgongoni. Vipele hivi hutokea wakati vishimo vya kupitisha jasho katika ngozi vinapozibwa kwa mafuta au seli za ngozi zilizokufa au wadudu yaani bacteria.
Maambukizi zaidi ya chunusi hutokea pale ambapo vijidudu yaani bakteria vinaposhambulia vishimo vilivyoziba; hapo kivimbe ambacho watu wengine huita upele hujitokeza pale ambapo Sebum, bacteria, seli za ngozi na seli nyeupe za damu zinapochanganyika na kujikusanya katika vishimo vya jasho vilivyoziba na eneo husika hupata vivimbe au vipele ambavyo tunaviita chunusi.
Magonjwa
Kuna wakati watu wanapata chunusi kwa sababu ya matatizo yanayohusiana na afya zao, unaweza kumkuta mtu ana upungufu wa baadhi ya vitamini au ana tatizo la kiafya linalopelekea apate matatizo kwenye ngozi mfano ukiwa na kisukari ni rahisi kupata chunusi. Ngozi yako ni kioo kinachoonesha mambo yanayoendelea ndani hauwezi ukawa na afya iliyokua dhaifu halafu utegemee ngozi iwe nzuri. Magonjwa yatokanayo na matatizo katika homoni (hormonal disorders) huongeza matatizo ya chunusi hasa kwa wasichana.
Madhara ya tokanayo na chunusi
Sura ya mtu baada ya kupata chunusi inaweza kumsababishia wasiwasi,
Kumpa kiwango cha chini cha kujithamini nakumfanya awe na mfadhaiko.
Upunguza mvuto wakati wakujamiana kwa watu waliokatika mahusiano
Kuondoa muonekano mzuri wa mtu katika uso wake
Kufanya mgongo wa mtu kukosa muonekano mzuri kutokana na kusambaa kwa chunusi hizi
Uweka dosari katika kifua cha mtu na hii mara nyingi uwapata wanaume na baadhi ya wanawake wachache.
Aina za madoa ya chunusi
Kuna aina 6 kuu za madoa zinazosababishwa na chunusi
Uvimbe uliojaa maji - aina kali zaidi ya doa inayosababishwa na chunusi; ni uvimbe mkubwa uliojaa usaha unaofanana na majipu na hubeba hatari kubwa ya kusababisha kovu la kudumu.
Vichwa vyeupe - vina mwonekano sawa na weusi, lakini vinaweza kuwa dhabiti na havitakuwa tupu vinapobanwa.
Madoa meusi - matuta madogo meusi au ya manjano ambayo yanakua kwenye ngozi; hayajajazwa na uchafu, lakini ni meusi kwa sababu utando wa ndani wa vinyweleo vya nywele hutoa rangi.
Paputi - matuta madogo nyekundu ambayo yanaweza kuhisi kama kidonda
Lengelenge - sawa na paputi, lakini ina ncha nyeupe katikati, inayosababishwa na mkusanyiko wa usaha.
Vinundu - uvimbe mkubwa ngumu ambao hujilimbikiza chini ya uso wa ngozi na inaweza kuwa chungu
Kama upo tayari kupokea ushauri ni kwa jinsi gani utaweza ufanya ili kuweka ngozi yako. katika muonekano nadhifu na wakupendeza na pia kama una chunusi utaweza kuziondoa kabisa. ni vyema ukatutafuta ili uweze kupata msaada kutoka kwetu. karibu kwa msaada